Headlines News :

Home » , » HAMAD RASHID ABWAGWA MAHAKAMANI

HAMAD RASHID ABWAGWA MAHAKAMANI

Written By Unknown on Thursday 29 November 2012 | 02:02

 
TUMESHINDA KESI YA AWALI AMBAYO MHE. HAMAD RASHID NA WENZIE WALIKISHTAKI CHAMA.

Hukumu imemalizika muda so mrefu hapa mahakama kuu.

Hoja zote za akina Hamad Rashid zimetupiliwa mbali.

Mahakama imejiridhisha kwamba, amri ya mahakama kuu ya kusitisha kikao cha BARAZA KUU kilichowafukuza uanachama HR na wenzake wanne haikufikishwa kwa chama kwa hivyo kikao husika kilikuwa halali.

Hii ina maana kw...amba OMBI la Hamad Rashid na mawakili wake kuwa WAJUMBE WOTE WA BARAZA KUU la CUF wafungwe jela kwa kukiuka amri ya mahakama limetupiliwa mbali.

Kesi ya msingi ambayo HR na wenzake waliifungua kupinga uhalali wa KAMATI YA MAADILI YA CHAMA itasikilizwa tarehe 28/01/2013 ambapo mawakili wa chama watapangiwa tarehe YA kuleta hoja za kutaka kesi ya msingi ifutwe kwa kuwa taratibu zote zilifuatwa na walifukuzwa kihalali na kwa kuzingatia katiba ya chama.

Chama chetu kimefurahishwa na uamuzi huu kwani unaonesha namna ambavyo hatukukurupuka.

Chama pia kinatoa pole kwa mhe. Hamad Rashid kwa kufiwa na mkewe mdogo jana, tutashiriki katika kutoa pole na mazishi pia. Tunaamini haya ya kimahakama yana nafasi yake na ya kibinadamu hayakwepeki.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Designed and Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr | 0719 625003/0765860437
Proudly powered by BONGO BLOG DESIGNERS
Copyright © 2012. HABARI BONGO - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template