Nakumbuka maneno ya MOHANDAS KARAMACHAND GANDHI
aliyefahamika sana kama MAHATIMA GANDHI na baba wa taifa la India, Yeye
alisema “SIWEZI KUHUBIRI AU KUPIGIA DEBE HARAKATI ZINAZOHATARISHA
UVUNJIFU WA AMANI KWASABABU SI MUHUMINI WAKE, NINACHOWEZA KUHUBIRI NA
KUKIPIGIA DEBE NI KUTOKUBALI KUMTII YEYOTE YULE ANAYEHATARISHA MAISHA
YAKO”
Hali inayoonekana Bukoba ni suala la utekelezaji wa miradi ya jamii
ambayo ipo kisheria lakini wapo wanaotaka kuitumia kama daraja la
kujitangaza, katika njia ya kuwaumiza wananchi kwasababu uwezi kufanya
mjadala usio na ugomvi kama upande mmoja hauna uhakika au hauelewi
kinachoendelea. Sasa je wana wa Bukoba wanajua nini kuhusu mikataba ya
soko na mtu akihoji katika hilo amekosea?
Kutokana na sintofahamu hiyo, wapo waliopewa idhini na wananchi kuhoji
kwa niaba yao, sasa wanapohoji waliopembeni na ambao hawajui lakini
wanataka kutumia daraja hilo kupata uongozi, tayari wanahubiri na
kupigia debe harakati zinazohatarisha uvunjifu wa amani kwasababu
wanajaza maneno kwa wasiojua mikataba ya soko iko je.
Inawezekana wakasema mengi kutokana na hisia, lakini hii inanipa picha
kwamba wasemao wanaweza kuamsha wasiyoyajua au kuyafanyia kazi, ila
kwasababu wanataka nafasi watayafanya makubwa ili kutimiza maandiko ya
wahenga kwamba “FAHARI WAWILI WAGOMBANAPO, NYASI NDIZO ZINAUMIA”.
Mbunge akisimama katika mikutao ya adhara anazungumzia siasa na
maenedeleo, mwalimu akiwa darasani anazungumzia masomo na taaluma husika
kulingana na kipindi.
Kagasheki kusema amemchonga Meya, kwa mtu mwenye uelewa na akili
timamu atajua amemaanisha nini lakini asiyejua chochote atajua
amemaanisha sura, lakini kagasheki angekuwa mwalimu, mimi ningeelewa
kuwa amemchonga meya kwakumfundisha somo Fulani ambalo limemfikisha
alipo.
Hivyo basi kwakuwa ni mwanasiasa Napata picha ya moja kwa moja kwamba
amemchonga kisiasa yaani amempa mwanga na mbinu za kusimama mbele ya
adhara na kuzungumza kwa kujibu hoja na jinsi gani anaweza kutetea
wananchi na hilo halina ubishi jamani waliokuwa bukoba tangu mapema
wanalijua, sasa utasemaje MUNGU AKAMUUMBA MTU KWA MFANO WAKE?
Tusidanganye wananchi.
Baba wa taifa na aliyeongoza mapinduzi ya taifa la China MAO TSE-TUNG
akiongoza chama cha kikomunisti kuanzia mwaka 1935, alisema kuwa
“MATABAKA UPAMBANA BAADHI HUSHINDA MAPAMBANO NLAKINI MENGINE HUSHINDWA,
NA HIVYO KUTOKOMEZWA NA NDIVYO HISTORIA YA USTAARABU ILIVYO DUNIANI”.
Sasa wanaochochea hasira na chuki kwa wananchi wakitumia nafasi ya
wananchi kutokuwa na makini au nafasi ya kusoma na kuelewa mambo, wajue
kwamba wanayoyakuza siku moja yatafutika kwasababu historia inaonesha
hivyo tangu karne zilizotangulia labda kama itakuwa mara ya kwanza
kushindikana, na inaonekana yakisha malizika waliokuwa upande Fulani
ulazimika kujipendekeza upande wa pili ili wapate nafasi.
Nawasihi kukumbuka maneno ya COMFUCIUS aliyezaliwa mwaka 551 BC na
kufariki 497 bc, alisema kuwa “FARAJA YETU KUBWA KATIKA MAISHA NI SI
KWAMBA BINADAMU KAMWE HATUANGUKI, BALI KILA TUANGUKAPO TUNAUWEZO WA
KUAMKA NA KUENDELEA NA SAFARI”, hivyo pamoja na mbunge kuwa ni nafasi
mojawapo ya ajira yake katika serikali ya jamhuri, bado anasemea
wananchi kupitia matukio anayoyashuhudia ambayo hata hivyo hayako sawa
katika maslahi ya mwananchi, kwahiyo wananchi walitaka azungumzie
chumbani ili muendelee kulishwa maneno ya uongo?
Kutokana na watu kuhitaji uongozi wa lazima, wanajitokeza wanaoibua
habari za uchochezi na kama tunavyotambua masuala ya UDINI hayana nafasi
kwa watanzania, kitendo cha mbunge kutoa usafiri kwa shughuli
mbalimbali kimekuwa kikifanyika tangu mbunge huyu amechukuwa madaraka ya
kuongoza jimbo la Bukoba na si kwa ajili ya kwenda kuhiji MUGANA pekee
bali hata kwenye shughuli za mazishi na hata kusafirisha maiti.
Zaidi ya yote mfano wa haraka mbunge ametoa usafiri kwa timu ya mpira
BUKOBA VETERAN kwenda Uganda ili kuiunga mkono timu ya taifa, mbona hiyo
hawazungumzi kuwa ni makosa? Yeye anapotoa fedha kwa ajili hiyo si
nafasi yake kusimamia kama kilichokodwa ni malori au tax hiyo ni kazi ya
waliokabidhiwa kitita.
Unaposisitiza kuwa mbona hajaenda MAKA ili aitwe alhaji nadhani ameona
gharama hiyo si sahihi kujinufaisha yeye bali wananchi wake kwasababu
kipindi hicho ndicho maeneo kadha ya jimbo yalikumbwa na upepo akatoa
msaada wa mabati kwa makanisa ya KYAKAILABWA na KILIMAHEWA pamoja na
chakula kwa waliokubwa na upepo ambao ulifikia zaidi ya milioni 5 ambapo
kwenda MEKA ni dola zaidi ya 900.
Kama kutoa msaada kanisani ni kosa mbona mabati hayajalalamikiwa?
Mwanafizikia wa kale duniani ALBERT EINSTEIN kutoka ULM WURTTEMBER
UJERUMANI, alisema “BINADAMU YEYOTE ANAYESOMA SANA NA AMBAYE HUTUMIA
KIDOGO MNO UBONGO WAKE MARA NYINGI HUANGUKIA KATIKA TABIA YA KIVIVU YA
KUFIKIRI” Nimesema hivyo kwasababu waliowengi wanaoonekana kupinga ni
wale wanaosoma sana na kupenda kuiga pasipokujipatia muda wa kufikiri
kwamba majimbo yanatofautiana.
Mbunge kupita kila siku anaenda kuudhuria vikao vya madiwani ni kweli
kwamba anatatua matatizo ya wananchi wake kama afanyavo Kagasheki? Ni
bora asijitokeze kila siku kmwenye vikao kama unavyopenda aige lakini
afanikiwe kuwafikia wananchi mapema na kutatu matatizo yao, lakini kama
zilivyo sheria za nchi, vikao vikifanyika ni lazima viwe na maandishi
ambayo kulingana na taratibu yatakwenda ngazi moja hadi nyingine katika
uongozi, je hayo yanafanyika katika vikao vya madiwani Manispaa ya
Bukoba?
Itakumbukwa tangu mwaka 2011 mbunge amekuwa akishiriki na hasa
akizungumza kupitia mikutano ya adhara kwa kuzungumzia miradi ya
maendeleo ikiwamo suala la kuvunja na kujenga soko kuu jipya la Bukoba,
ambapo iko katika ushirikiano wa pamoja, lakini kwakuwa kila kitu kina
ngazi yake imekuwa ni kawaida Meya akaratibu baadhi ya masuala lakini ni
lazima atoe taarifa kupitia vikao na hata kuwasilisha vielelezo kwa
mbunge, ila amekuwa hafanyi hivyo na hilo ndo lalamiko la Kagasheki
baada ya kuonekana baadhi ya madiwani nao wakihoji lakini wakiogopa
kutokana na ubabe wa meya, wakisubiri Kagasheki aulize ambapo inaonekana
wamemtoa kama chambo kwa Meya na wananchi.
Hali hiyo inanionesha na kunikumbusha maneno ya mtunzi maarufu wa kale
AGATHA CHRISTIE kupitia kitabu chake cha THE MAN IN THE BROWN SUIT,
aliyesema kuwa “NI MAISHA MAGUMU NA AJABU, MWANAUME HAWEZI KUOA MWANAMKE
KAMA HANA SURA NZURI NA HAVUTII, NA MWANAMKE HATAMPENDA MWANAUME MWENYE
SURA NZURI KUMZIDI NA ANAYEVUTIA”
Kupitia maneno hayo, wananchi watajua nani wanamtaka ili awaongoze na
wanampenda wala si vema mtu kujipendekeza katika hilo, wakati mambo
muhimu yanafichwa nyumbani mwa familia ya Meya, watu watajuaje? Mbunge
akiuliza hilo mnamkandamiza?.
Ya Mungu mpe mungu nay a Kaizali mpeni Kaizali, Balozi HAMIS KAGASHEKI
unapigana na wananchi wako ila wanaokusakama wanataka nafasi tu, ila
kwasababu hawana jinsi wametafuta namna ya kukuchafua.
Mwanafalsafa SOCRETS wa ITALIA katika miaka ya 500-400 kabla ya
Kristo, alisambaza elimu kupitia maandiko akiwataka wananchi kusimama
kidete katika maslahi yao, lakini waliokuwa na uchu wa madaraka
wakiongozaz wananchi mbumbumbu, baada ya kuona Socret anatoa elimu na
wananchi wanapata mwamko, walimlazimisha ajiue kwa kunya sumu mwenyewe,
lakini kabla hajainywa alisema “VIONGOZI WENYE TAMAA WAMEAMUA KUUA
KICHWA KIMOJA, LAKINI WAMESHINDWA KUJUA KWAMBA NIMEKUFA MIMI ILA ELIMU
YANGU IMEJAA TAYARI VICHWANI MWA RAIA, HIVYO WATAENDELEZA MAPAMBANO NA
KUJIKOMBOA KUTOKA MIKONONI MWA UBWENYENYE”
Kagasheki hata wakikufitini kisiasa hawa wenye tamaa, naamini ujumbe
wako tayari wananchi wameupata na kwasasa wanajua kudai haki na ndo
maana baada ya tamko lako kwenye mkutano wa hdahara tarehe 24 november
2012 ulisema soko halijafanyiwa upembuzi yakinifu hivyo halitabomolewa
kwa haiwezekani ukajenga sehemu usiojua kiasi cha maji chini ya ardhi.
Ndipo siku moja baadaye ikiwa ni jumapili, kampuni isiyojulikana
inayojiita GEOPINIUS INVESTMENY iliyoandikwa kwa MAKERPEN ubavuni mwa
gari aina ya FUSO T675 AEJ kutoka Dar es salaam kwa mujibu wa
(kandayaziwaleo.blogspot.com) ya huko Bukoba, ilikuja na mashine za
kuchimba na kupima kiasi cha maji ndani ya soko kuu, lakini kwa akili
uliowapa wananchi wakatambua haki yao walizuia gari hiyo kwani Kesi ya
soko bado iko mahaklamani, je anayesema soko lazima livunjwe amepanga na
mahakama kwamba lazima ashinde kesi hiyo na mbona anataka kulivunja
kabla ya machi ambapo kesi inasikilizwa tena?
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !