Headlines News :

Home » , , » Rais Obama amkashifu Romney kwa ubaguzi

Rais Obama amkashifu Romney kwa ubaguzi

Written By Unknown on Tuesday, 20 November 2012 | 03:53

Rais wa Marekani Barack Obama amemshtumu mpinzani wake wa chama cha Republican, katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa urais wa mwezi Novemba Mitt Romney, kwa kubagua sehemu kubwa ya raia wa Marekani.

Bwana Romney alinaswa kisiri kwenye ukanda wa video akitoa matamshi ya kuwadharau baaadhi ya wapiga kura wakati wa hafla ya faragha ya kuchangisha pesa za kampeni katika chama cha Republican.

Akizungumza kwenye mahojiano na kipindi kimoja cha televisheni nchini Marekani Obama amesema jambo ambalo amejifunza akiwa rais ni kuwatumikia wamarekani wote.

Baada ya kuchaguliwa , alisema , atajitahidi kuwahudumia hata wale ambao hawakumpigia kura.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

 
Designed and Bloggerized by | Tryphone Chasama Jr | 0719 625003/0765860437
Proudly powered by BONGO BLOG DESIGNERS
Copyright © 2012. HABARI BONGO - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template